HAIKI YA KUTEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA IRENTE - LUSHOTO
Tarehe 12/8/2017 siku ya vijana duniani; maskauti wa shule ya sekondari Ubiri walifanya haiki ya kutembelea kituo cha watoto yatima Irente. Maskauti hawa walitembea yapata kilometa 18 ili kufanikisha jambo hili. Kituoni hapo maskauti walifanya shughuli mbalimbali kama vile usafi, kunyoosha nguo za watoto pamoja na kucheza na watoto hao. vilevile walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusu kituo hicho kilivyoanza, namna kinavyowapata watoto hao na kuwalea pia kuwaendeleza. kwa ufupi tulijifunza mambo mengi sana pamoja na kufurahia safari yetu.